Saturday, August 21, 2021

Video ya salamu za kichaga

Bofya hapo chini kutazama na kusikiliza video ya salamu ya kichaga






MAWASILIANO

Tell+255 621 058168=whattsapp

sirgeorgeboazndeyanka09@gmail.com

Google: Mwalimu george boaz 

facebook: sirGeorge Boaz 

HAI

KILIMANJARO

UTANI WA WACHAGA

Leo napenda kuwapa utani wa wachaga: Please usikasirike ni utani tu wenzangu.


 

ü  WAROMBO:

Warombo ni wajanja sana kibiashara/wezi pia, wanapenda dili za magendo mno. Ni walevi sana kuliko ma wachaga wengine, huwapeleka wake zao kijijini wanapoleta kujua mjini. Wanaume wa rombo wanachunwa sana na wanawake wa marangu na wanawaita “Vishohia”  

Wanawake wa rombo ni mama huruma sana huwa hawakatai. Ukioa mrombo ujue umeolea wenzako.

Wanaume wa rombo hawawezi kuridhisha wapenzi wao jambo linalopelekea kuchepuka na kuomba msaada/Jeshi la uokoaji na unusuruji wa ndoa Kenya.

Ni utani tu wenzangu Warombo ila mbadilike.

ü  WAMARANGU:

Wanawake wa marangu ni wazuri sana wa umbo na sura ya kuvutia kuliko wachaga wengine wote. Lakini wanawachuna sana warombo, Wanawake wa marangu wana dharau sana na wanaume wa wa kimarangu ni waoga na washamba kuliko wanawake wao. Mwanamme wa kimarangu kupigwa na mke si jambo la ajabu maana wanadundwaga sana.

Ni utani tu wenzangu Wamarangu ila mbadilike. Ngaichoka kabsa na shindo icho.

ü  WAKIBOSHO:

Wanafanana sana na warombo kwa asilimia nyingi kuanzia unywaji wa pombe na mengineyo. Lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni kuchinja… wengi wao wanamiliki mabucha. Wana hasira sana na ni wakatili sana… Mkibosho kukuchoma kisu sio jambo geni kwao na siku ya mazishi anakuja kudai kisu chake.  Usilete utani wala michezo na hawa watu maana kisu kitakukuta…. “nka kyandu”

Ni utani tu wenzangu Wakibosho ila mbadilike. Kukapa kyandu…kudosha kyandu…

ü  WAMACHAME:

Aisee hawa ni wezi sana ni watapeli mno, Ukifanya nae dili umeliwa. Ni wasiri sana lakini wako makini sana kwenye maswala ya noti. Mmachame anaweza kukuua akiwa anatabasamu, sio waaminifu sana Ila ndio wachaga wanaoongoza kwa kwenda kanisani mara nyingi sana kuliko wenzao.

Wanawake wa kichaga huitwa “wapalestina” Inaaminika huwauwa waume zao wanapotajirika ili warithi mali. Wanawake hawa hawana umbo na sura ya kuvutia sana kama wachaga wengine, Wanapenda sana Uongozi wa kanisa na umaarufu kwa kujiita “Mangi” katika duka zao.

Ni utani tu wenzangu Wamachame ila mbadilike. Kutambashueny da ro wanawama’….

ü  WAURU:

Hawa hupenda kusoma lakini hawana maendeleo kabisa. Hadi leo eneo la “kishumundu” ni kama kiashiria cha wachaga washamba.  Wanawake wakifikia miaka 40 huwa wehu na wanaume huwa vichaa mapema zaidi. Wanaume ni  wavivu lakini wanawake ni wachapakazi hodari. Wanazurura mjini na mabeseni yenye ndizi mbivu ukioa huru jiandae kulea…………

Ni utani tu wenzangu Wuruila mbadilike sasa.

ü  WASIHA:

Kwanza hawapendi kuitwa wachaga wanajiitaga watu wa west-kilimanjaro, Ni mchanganyiko wa wameru na wamasai. Hawapendi shule ila wanapenda zaidi kazi za ufundi na kilimo. Viazi vingi vya chips hutoka kwao, Wanawake zao wana vigimbi sababu ya kulima mno na kupanda panda vilima.

Ukitaka kuoa mkulima mzuri ambae ajapitia shule ila ni bora kuliko wa SUA nenda SIHA…

Ni utani tu wenzangu Wasiha ila mbadilike kidogo sasa.

ü  WAKIRUA:

Wanapenda sifa kama wahaya,  Wanawake wa kirua ni wachawi kupindukia… wanaloga hata  jiwe ili tu alikomoe. Wanaume wa kirua hawapendi kuoa kwao, Hawapendi kuishimjini wanaogopa gharama… lakini siku wakija mjini wawili utadhani wako mia maana sio kwa kelele hizo….

 

Ni utani tu wenzangu Wakirua  ila mbadilike.

ü  WA OLD-MOSHI:

Hawa ni mafundi stadi wa ujenzi wa nyumba japo hawajengi kwao. Mpaka leo hamna daladala ya kwenda old-moshi inayoanzia moshi mjini. Maana ni wabishi kulipa nauli na pesa inaishia kwenye mbege njiani. Wanaume wamezoea kutoka nyumbani saakumi na moja alfajiri na kurudi saa sita ya usiku kwa miguu.

Ni utani tu wenzangu Wa old-moshi ila mbadilike.

 

 

 MAWASILIANO


Tell+255 621 058168=whattsapp

sirgeorgeboazndeyanka09@gmail.com

Google: Mwalimu george boaz 

facebook: sirGeorge Boaz 

HAI

KILIMANJARO