Saturday, August 21, 2021
Video ya salamu za kichaga
UTANI WA WACHAGA
Leo napenda kuwapa utani wa wachaga: Please usikasirike ni utani tu wenzangu.
ü WAROMBO:
Warombo ni wajanja sana kibiashara/wezi pia, wanapenda dili za magendo mno. Ni walevi sana kuliko ma wachaga wengine, huwapeleka wake zao kijijini wanapoleta kujua mjini. Wanaume wa rombo wanachunwa sana na wanawake wa marangu na wanawaita “Vishohia”
Wanawake wa rombo ni mama huruma sana huwa hawakatai. Ukioa mrombo ujue umeolea wenzako.
Wanaume wa rombo hawawezi kuridhisha wapenzi wao jambo linalopelekea kuchepuka na kuomba msaada/Jeshi la uokoaji na unusuruji wa ndoa Kenya.
Ni utani tu wenzangu Warombo ila mbadilike.
ü WAMARANGU:
Wanawake wa marangu ni wazuri sana wa umbo na sura ya kuvutia kuliko wachaga wengine wote. Lakini wanawachuna sana warombo, Wanawake wa marangu wana dharau sana na wanaume wa wa kimarangu ni waoga na washamba kuliko wanawake wao. Mwanamme wa kimarangu kupigwa na mke si jambo la ajabu maana wanadundwaga sana.
Ni utani tu wenzangu Wamarangu ila mbadilike. Ngaichoka kabsa na shindo icho.
ü WAKIBOSHO:
Wanafanana sana na warombo kwa asilimia nyingi kuanzia unywaji wa pombe na mengineyo. Lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni kuchinja… wengi wao wanamiliki mabucha. Wana hasira sana na ni wakatili sana… Mkibosho kukuchoma kisu sio jambo geni kwao na siku ya mazishi anakuja kudai kisu chake. Usilete utani wala michezo na hawa watu maana kisu kitakukuta…. “nka kyandu”
Ni utani tu wenzangu Wakibosho ila mbadilike. Kukapa kyandu…kudosha kyandu…
ü WAMACHAME:
Aisee hawa ni wezi sana ni watapeli mno, Ukifanya nae dili umeliwa. Ni wasiri sana lakini wako makini sana kwenye maswala ya noti. Mmachame anaweza kukuua akiwa anatabasamu, sio waaminifu sana Ila ndio wachaga wanaoongoza kwa kwenda kanisani mara nyingi sana kuliko wenzao.
Wanawake wa kichaga huitwa “wapalestina” Inaaminika huwauwa waume zao wanapotajirika ili warithi mali. Wanawake hawa hawana umbo na sura ya kuvutia sana kama wachaga wengine, Wanapenda sana Uongozi wa kanisa na umaarufu kwa kujiita “Mangi” katika duka zao.
Ni utani tu wenzangu Wamachame ila mbadilike. Kutambashueny da ro wanawama’….
ü WAURU:
Hawa hupenda kusoma lakini hawana maendeleo kabisa. Hadi leo eneo la “kishumundu” ni kama kiashiria cha wachaga washamba. Wanawake wakifikia miaka 40 huwa wehu na wanaume huwa vichaa mapema zaidi. Wanaume ni wavivu lakini wanawake ni wachapakazi hodari. Wanazurura mjini na mabeseni yenye ndizi mbivu ukioa huru jiandae kulea…………
Ni utani tu wenzangu Wuruila mbadilike sasa.
ü WASIHA:
Kwanza hawapendi kuitwa wachaga wanajiitaga watu wa west-kilimanjaro, Ni mchanganyiko wa wameru na wamasai. Hawapendi shule ila wanapenda zaidi kazi za ufundi na kilimo. Viazi vingi vya chips hutoka kwao, Wanawake zao wana vigimbi sababu ya kulima mno na kupanda panda vilima.
Ukitaka kuoa mkulima mzuri ambae ajapitia shule ila ni bora kuliko wa SUA nenda SIHA…
Ni utani tu wenzangu Wasiha ila mbadilike kidogo sasa.
ü WAKIRUA:
Wanapenda sifa kama wahaya, Wanawake wa kirua ni wachawi kupindukia… wanaloga hata jiwe ili tu alikomoe. Wanaume wa kirua hawapendi kuoa kwao, Hawapendi kuishimjini wanaogopa gharama… lakini siku wakija mjini wawili utadhani wako mia maana sio kwa kelele hizo….
Ni utani tu wenzangu Wakirua ila mbadilike.
ü WA OLD-MOSHI:
Hawa ni mafundi stadi wa ujenzi wa nyumba japo hawajengi kwao. Mpaka leo hamna daladala ya kwenda old-moshi inayoanzia moshi mjini. Maana ni wabishi kulipa nauli na pesa inaishia kwenye mbege njiani. Wanaume wamezoea kutoka nyumbani saakumi na moja alfajiri na kurudi saa sita ya usiku kwa miguu.
Ni utani tu wenzangu Wa old-moshi ila mbadilike.
-
Majina ya wanawake. Ikunda = upendo Anansia = anafuraha Aikande = asante baba Anaufoo = ana upole Aika = asante Nsia = furaha A...
-
KWA NINI WANAUME WA KICHAGA HUFA MAPEMA KULIKO WAKE ZAO... Jambo hili la wanaume wa kichaga hususani machame kuanza kufariki kabla ya wake z...
-
Fonolojia ya kimachame na kiswahili: na mwandishi George Boaz swai na zabron Kabila la wachaga ni kabila ambalo linapatikana mkoani Kili...
-
Mama=nkyeku Baba=mmiku AINA ZA SALAMU ZA KIMACHAME kwifo ndesa vamashami vakwidikira VIPI =nyinda,Mbonyi, NAMBIE =shivya
-
kwalolya na mashora mbuya yakwa kwifyenda? Kukundee ikuloshaa iidikira kwa kimashamii? embu eta mariso daa-te Maneno ya kichaga (kimachame...
-
KOO MAARUFU ZA WACHAGA Majina ya ukoo ni moja kati ya utambulisho wa sehemu wanapotoka katika mikoa mingine au kabila. KOO MAARUFU...
-
MISEMO YA KICHAGA 100 (machame) NA MAANA YAKE Fyaaso makumii iyana fya kimashami. maneno ya kichaga cha machame na maana yake. Kwanza natan...
-
WANAWAKE mtoto wa kwanza wa kike anaitwa mammi/mae ya mmi (kimachame) ikimaanisha mama yake mume(mzawa wa kike mtaja mama wa mume) mtoto wa ...
-
HISTORIA YA KABILA LA WACHAGA, WACHAGA, Ni moja ya makabila yanapatikana katika nchi/Taifa la TANZANIA, Ni kabila la watu wenye as...
-
AWAMASHANI NKWI VAUKYE NAFO? Niyinda mbuya yakwa: Mbandu vavii veuka efoo ifumbuu lya usambara vakasha veryani na mae waawo na vakavawo. Van...