KARIBU TANGA:
Na
mwandishi GEORGE BOAZ.
Tanga ni moja ya mikoa inayounda nchi ya Tanzania, Mkoa huu unapatikana kaskazini mwa Tanzania. Tanga ni moja ya mikoa yenye historia ya kipekee sana nchini Tanzania, Mkoa huu umeundwa na wilaya 10 (kumi) huku ukikadiriwa kuwa na km 27,348 na makao makuu yake yakiwa ni Tanga mjini.
Tanga insaemekana imeanzishwa
na wafanyabiashara Waajemi katika karne ya 14 BK. Tanga ni mji ambao sifa zake zilianza
kusikika kuanzia enzi za utawala wa Wajerumani,
jiji ambapo shule ya kwanza ya serikali ilijengwa
enzi hizohizo za utawala wa Wajerumani, jiji ambalo liliendelea kukua sana
kutokana na kilimo cha katani na
hivyo kukusanya vijana toka kila kona ya nchi kuja kutafuta kazi katika mashamba makubwa
ya katani wakati huo.
Tanga ni moja pia ya mikoa ulio fukoni
mwa Bahari ya Hindi wenye Postikodi namba 21100.
Tanga ndio mkoa pekee unaosifiwa
kuwa ndiko mapenzi yalipozaliwa je? Ni
ya kweli, Tuambatane katika makala hii fupi kuhusu Tanga.
Yaliyomo:
·
HISTORIA YA TANGA.
·
USAFIRISHAJI.
·
UTALII.
·
KILIMO NA VIWANDA.
·
WAKAZI.
·
ENEO.
·
SANAA.
·
MENGINEYO.
HISTORIA YA TANGA:
Kama tulivyokwisha kutazama kwa
uchache historia ya mkoa wa Tanga hapo juu. Tanga ni mkoa wenye historia ya
kipekee katika Nyanja zote. Tukisema tuelezee muda hautatosha kwa maana ni
hadithi ndefu kusimulia.
Tanga ni Jina la mji wa Tanga linaaminiwa
kutokana na lugha ya Kibondei yaani
Shamba, kwa sababu wenyeji ambao walikuwa Wabondei waliishi kisiwa cha Toten lakini shughuli zao za kilimo walizifanyia
eneo ambalo kwa sasa linajulikana kama mji wa Tanga.
USAFIRISHAJI:
Katika suala la ubebaji na
usafirishaji Tanga imebarikiwa kuwa na aina zaidi ya tatu za usafirishaji.
Tunaweza sema jiji la tanga ni moja ya mikoa ambayo unaweza kufika kwa njia
mbalimbali.
Kwanza Tanga ina usafirishaji wa
barabarani unaounganisha mkoa wa Kilimanjaro na wa pwani kupitia same na
korogwe. Pili ni usafirishaji wa njia ya reli unaotoka Tanga kwenda Kilimanjaro
mpaka Arusha, na tanga kwenda Dar es salaam kupitia Pwani. Tatu ni usafirishaji
wa anga unaotoka kiwanja cha ndege tanga kwenda viwanja vingine vya ndege. Nne
ni usafirishaji wa majini ukihusisha Bandari ya KASELA tanga inayotoa huduma
kwenda bandari nyingine kama bandari ya dar e s salaam
UTALII:
Mkoa wa Tanga una maeneo ya
kitalii yanayoweza kuwavutia watalii wengi ndani na nje ya Tanzania, Hasa
kutokana na ukarimu wa watu wake. Watu wa Tanga wanasifika kuwa na haiba ya
ukarimu kama walivyo watanzania wengi jambo ambalo linaweza kuwa kivutio kwa
watalii wengi kutembelea mkoa huo. Kwa kawaida ukarimu huwavutia watalii wengi,
Na kuwajengea hali ya usalama na kujifunza mengi kutokana kwa wenyeji wao.
Mkoa wa tanga umebarikiwa kuwa na
vivutio vingi vya utalii ambavyo husaidia katika kukuza pato la Nchi na la mkoa
huo. Mbali la pato vivutio hivyo husaidia kuleta fedha za kigeni na kuufanya
mji huo kukua. Mojawapo ya vivutio hivyo ni Amboni caves, kisiwa cha Toten, Magofu ya Tongoni, Kisiwa cha ulenge, Sakarani
makaburi ya vita kuu ya kwanza ya dunia, Mbuga ya wanyama saadani, Mto pangani,
Msitu wa Magoroto, Mbuga ya mkomanzi, Urithi
Tanga museum na fukwe za bahari zenye upepo mwanana.
KILIMO NA VIWANDA:
Kama ilvyo kwa mikoa mingine hapa
Tanzania hulima ndivyo ilivyo kwa mkoa wa Tanga, Tanga hutegemea kilimo cha
riziki, uvuvi na ufugaji.
- Tanga hulima mazao ya chakula kama vile,
Mahindi, Maharage na mihogo. Huku mazao ya biashara yakiwa ni ni katani, pamba, kahawa, chai, nazi, tumbaku na korosho. Katika ufugaji wakazi wa tanga hufuga ng'ombe, mbuzi na kondoo pamoja na kuku.
- Katani ilikuwa zao la biashara hasa kwa ajili
ya Tanga tangu kuingizwa kutoka Mexico zamani
za Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.
Hulimwa kote mkoani isipokuwa Lushoto, hasa Muheza na Korogwe kwenye
mashamba makubwa. Mashamba hayo yalikuwa ya walowezi, yakataifishwa baada ya uhuru. Tangu kuanguka kwa sekta ya umma yamebinafsishwa
tena siku hizi. Zao la katani linategemea sana soko la dunia,
umuhimu wake ulirudi nyuma tangu miaka ya 1960.
Tanga ilikuwa na viwanda vingi kiasi katika miaka ya 1960 na 1970 lakini karibu vyote vimekwama kutokana na siasa ya Ujamaa na uchumi wake ulioiga mfumo wa nchi za kisoshalisti. Viwanda vichache
vilivyobaki havizalishi mali kulingana na uwezo wao. Kilichobaki hasa ni
kiwanda cha saruji Tanga.
Mkoa wa Tanga ulikuwa na viwanda vingi sana hii ni
kutokana na kuwa katika ukanda wa pwani ambapo watu toka magharibi waliweza
kufikia hapo kwa haraka kuliko mikoa mingine ya Tanzania, Ujio wa watu wa
magharibi walifanya jiji la Tanga kukua haraka na kuwa na viwanda vingi vyenye
kuzalisha bidhaa mbalimbali kama vile, Saruji, Mafuta ya kupakana bidhaa
nyinginezo nyingi.
Pia mkoa wa Tanga umekuwa maarufu kwa umekuwa maarufu kwa
kilimo cha Mkonge na matunda matunda pia kuna viwanda vya uchakataji wa mkonge
na usindikaji wa matunda.
WAKAZI:
Mwaka 2012 wakazi waliohesabiwa katika sensa walikuwa 2,045,205[1].
Makabila makubwa
mkoani Tanga ni Wasambaa, Wazigua, Wabondei na Wadigo.
Mengine ni Wapare, Wataita, Wambugu, Wasegeju na Wanago.
Pia kuna Waarabu wengiwengi
wenye asili ya Oman.
Wasambaa ndio kabila kubwa
lililoko katika milima ya
Usambara, Muheza, Korogwe na Lushoto.
Kwa jumla ndio asilimia 40
ya wakazi wote wa mkoa.
Wazigua ni kabila kubwa
huko Handeni na
sehemu za Korogwe na Pangani. Wabondei wako hasa Muheza na sehemu za
Pangani. Wadigo ndio wengi Tanga yenyewe na sehemu za pwani.
ENEO:
Tanga ni kati ya mikoa midogo ya Tanzania ikiwa na msongamano mkubwa wa wakazi ndani ya eneo lake.
Msongamano ni mkubwa hasa wilaya ya Lushoto kwenye ardhi yenye rutuba nzuri.
Mkoa una eneo la km² 27,348 ambalo linaunganisha sehemu
za pwani pamoja
na milima ya
ndani kama Usambara.
Eneo linalofaa kwa kilimo ni
km² 17,000.
Kuna wilaya 10
ambazo ni Handeni Vijijini, Handeni
Mjini, Kilindi, Korogwe
Vijijini, Korogwe
Mjini, Lushoto, Mkinga, Muheza, Pangani na Tanga Mjini.
SANAA:
Nanukuu; “Tanga ni mji ambao sifa
zake zilianza kusikika kuanzia enzi za utawala wa Wajerumani,
jiji ambapo shule ya kwanza ya serikali ilijengwa
enzi hizohizo za utawala wa Wajerumani, jiji ambalo liliendelea kukua sana
kutokana na kilimo cha katani na
hivyo kukusanya vijana toka kila kona ya nchi kuja
kutafuta kazi katika mashamba makubwa
ya katani wakati huo.
Tanga ni mji ambao kutokana na
wingi wa vijana wakati huo, shughuli za burudani ya muziki nazo
zilifikia kiwango cha juu kuliko sehemu nyingi Tanzania.
Ukizungumzia historia ya muziki wa dansi, huwezi kukwepa kuzungumzia Tanga, kwani
historia inatueleza kuwa kabla ya kuanza vikundi vya muziki wa dansi
kulianzishwa klabu za kucheza dansi. Klabu hizo zikitumia muziki wa santuri, wanachama wake walicheza na hata kushindana
kucheza muziki kwa mitindo mbalimbali ya kigeni
ikiwemo waltz, tango, chacha, rumba na kadhalika.
Klabu za kwanza nchini zilianzia
Tanga. Kulikuwa na klabu kama Young Noverty miaka michache baada ya Vita ya
Kwanza ya Dunia, wakati huo
nchi ya Tanganyika ikiwa
bado changa kabisa. Mtindo huu wa vilabu vya dansi ulienea na baadaye kuingia
Dar es Salaam na miji mingine iliyokuwa imeshaanza wakati huo. Vilabu hivi
ndivyo baadaye vilivyanzisha vikundi vya kwanza vya muziki wa dansi. Hata
majina ya vikundi hivyo vya kwanza yalihusiana na klabu za burudani za wakati
huo. Kulikuwa na vikundi kama Coast Social Orchestra, Dar es Salaam Social
Orchestra na kadhalika.
Hivyo mji wa Tanga ulikuwa
katika ndoto za
vijana enzi hizo. Kwa vile vijana wengi walikusanyika katika jiji hilo,
kulianzishwa pia klabu ambazo zilikuwa kwa ajili ya vijana waliokuwa
wakitoka kabila moja. Klabu hizo zikiwa na nia ya
wanachama wao kusaidiana katika shida na raha, na vilabu hivyo pia vilikuwa
sehemu muhimu katika kutoa burudani kwa vijana waliotoka sehemu moja.
Kati ya klabu hizo kulikuweko na
klabu iliyoitwa Young Nyamwezi: kama jina lake lilivyo ilikuwa klabu ya vijana
kutoka Unyamwezi. Hatimaye mwaka 1955 klabu hiyo ilianzisha bendi yake iliyoitwa Young
Nyamwezi Band, bendi hiyo ilikuja kukua na
baada ya uhuru ilibadili
jina na kuitwa Jamhuri Jazz Band. Hakika kwa vijana waliokuwa wapenzi wa
muziki miaka ya 1960 na 1970 ilikuwa
lazima uifahamu Jamhuri Jazz Band, muziki wake, au kwa lugha ya enzi zile,
‘vibao’ vyake vilivyojulikana Afrika ya
Mashariki nzima. Bendi hiyo ilikuwa
ikibadili mitindo ya upigaji wake na kupiga katika
mitindo ya ‘Toyota’ na hatimaye ‘Dondola’. Aliyekuja kumiliki bendi hiyo,
ambayo wapenzi wake pia waliita JJB alikuwa Joseph Bagabuje, kulikuwa hata
maelezo wakati fulani kuwa JJB ilikuwa kifupi cha
Joseph Jazz Band na si Jamhuri Jazz Band. Kama ilivyokuwa kawaida ya bendi za
wakati ule Jamhuri Jazz Band ilisafiri sana na kufanya maonyesho katika kila
kona ya nchi, jambo hilo pamoja na kuwa bendi hii ilirekodi na kutoa santuri
kupitia kampuni za kurekodi za Kenya na pia kurekodi nyimbo zake
katika radio ya Taifa uliifanya bendi hiyo kuwa maarufu sana.
Upigaji wa aina ya pekee wa gitaa la rhythm wa bendi hii, ambao
uligunduliwa na Harrison Siwale, maarufu kwa jina la Sachmo, uliigwa na wapiga
gitaa ya rhythm wengi nchini. Uimbaji wa kutumia waimbaji wawili
tu, uliopendelewa na bendi za Tanga wakati huo ikiwemo bendi nyingine maarufu
ya Atomic jazz
Band, ulikuwa wa aina yake pia.
Jamhuri Jazz Band pia ndiyo
ilikuwa chanzo cha bendi maarufu ya Simba wa
Nyika. Inasemekana kuwa siku ambayo
Jamhuri Jazz Band ilikuwa imekodishwa kwa ajili ya kupiga kwenye harusi kule Muheza. Wanamuziki walikuwa wakilazimika kukusanyika
katika jengo la
klabu lililokuwa Barabara ya 15 ili kupata usafiri wa
kwenda Muheza.
Siku hiyo wanamuziki wengine walikusanyika lakini George na Wilson Peter, Luza
Elian na wengine wachache hawakuonekana. Baada ya upelelezi mfupi ikajulikana kuwa wamejificha au
wameondoka mjini Tanga, hivyo ikalazimika kutafuta wanamuziki viraka wa
harakaharaka kuweza kufanikisha onyesho la siku hiyo.
Kwa karne hii ya 21 Tanga pia
inao wasanii maarufu ndani na nje ya Tanzania wanaojulikana maarufu kama Sumalee, Cpwaa{halifa
ilunga}, Matonya{Sefu Shabani}, Kassim Mganga, Wagosi wa Kaya, Ring 2be aka
Pete{Rashidi Ngayama}, Mwana FA{Hamisi
Mwinjuma}, Bwana Misosi, Q Chilla{Abubakari Katwila}, MB Doggy, R.O.M.A{Ibrahim
Mussa}, Top C, Dr Karim, John Walker, Gelly wa rhym, Hemed Phd{Hemed Suleiman}, Sharomillionear{Mohamed
Mtikey},Danny Msimamo Pia waigizaji maarufu kama hayati King
MAJUTO walitokea mkoa waTanga.
Tanga na mapenzi ni hadithi
isiyoweza simulika pasi na kupata wasaa wa kuonya utamu huu kwa kuishi katika
jamii hii au kuoa/kuolewa tanga kwani wahenga walisemaa raha ya ngoma uingie
ucheze.
Kutokana na maelezo hapo juu
kuhusu simulizi ya mkoa huu, Vijana wengi walivyopenda kwenda tanga kwani ndio
mji uliokuwa umeendelea na ulikuwa na ustaarabu wa magharibi ulifanya suala la
mapenzi kuongezeka. Hii ni kutokana na mwingiliano
wa makabila pia uwepo wa utamaduni wa ngambo(wazungu na waarabu)
NB: Wakenya huwa na msemo wa Mombasa raha, na ukija ukiangalia kijiografia Mombasa na
Tanga imepakana na zote zipo uwanda wa pwani.
Kuwepo kwa starehe na burudani kiasi cha kusifiwa ni matokeo ya Miji
hiyo kuendelea mapema kabla ya mingine huku ikiwa na miingiliano ya tamaduni
toka ndani na nje ya mipaka yake. Pia kuwepo na ustaarabu wa ngambo ya
magharibi.
MENGINEYO:
Salamu maarufu ya wakazi wa Tanga
ni
NENO |
TAFSIRI |
1. Assalam Alaikum |
Amani iwe na wewe |
2. Onga makeo |
Habari za asubuhi. (kisambaa) |
Kutokana na Tanga kuwa na
makabila zaidi ya moja uwepo wa salamu mama hamna. Zaidi hutumia salamu ya dini
ya kislamu kutokana na wakazi hao wengi kuwa wafuasi wa dini hiyo.
Bwana yesu asifiwe ni chache
hivyo unaweza kutumia lugha ya taifa
kutoa na kuitikia salamu.
Facebook: SirGeorge Boaz
No comments:
Post a Comment
061058168